YALIYOMO YAMO BLOG

Habari kila kona

Friday, 5 December 2014


Na Karoli Vinsent

     WAKATI Rais Jakaya Kikwete akisuasua kuwachukulia hatua viongozi waliotajwa na Bunge kuhusika Katika Wizi wa zaidi ya Bilioni 320 kwenye Akaunti ya Tegeta Esrcow ,naye Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila Ameibuka upya na Ameivaa Ikulu 

       Baada ya kusema Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete inamedhamilia kuwalinda wezi waliohusika katika kuiba pesa hizo,baada ya kumzuia Mkurugenzi wa ofisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa PCCB Dk Edward Hosea kutoiwasilisha Taarifa ya uchunguzi juu ya sakata hilo la Esrcow  kwa Umma kutokana na Ripoti ya PCCB kuwataja vigogo wa Ikulu kuhusika katika kuchota pesa kwenye Benk ya Stabink.

    Hayo yamebuliwa mda huu Jijini Dar es Salaam na Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo Kafulila  huku akizungumza kwa uchungu alisema Inasikitisha kuona jinsi Ikulu inavyotumia ubabe wake kumzuia Dk Hosema kutoiweka wazi ripoti yake ya uchunguzi.
   “Tunafahamu wazi serikali inataka kuwalinda watu waliochota pesa,kutokana na kitendo chake kumzuia PCCB asiweka hadharani ripoti kwa kisingizia uchunguzi ujakamilika,ujakamilika kivipi wakati tunakumbuka wazi Mkurugenzi wa PCCB Dk Hosea wakati kongamano la SADC  kuhusu Rushwa  uliofanyika mkoani mwanza mwezi Novemba”
“Alisema ripoti yake ya uchunguzi kuhusu Akaunti ya Escrow umekamilika na tayari wameshamkabidhi Waziri Mkuu ingawa waziri huyo mkuu alikana,na hii yote inafanyika hivi ni kutokana na Ripoti ya PCCB kuwepo  na majina ya Vigogo wa Ikulu ambao walichota pesa kwenye Benki ya Stabink”alisema Kafulila
      Kafulila aliongeza kuwa leo majina ya watu waliochota pesa kwenye Benki ya Mkombozi tu wanatajwa ,huku wengine kwenye Benki ya Stabink Benki wakiachwa kwakuwa ni vigogo wa Ikulu.
      “Leo majina ambao kamati ya PAC waliyopewa na PCCB ni ya Benki ya mkombozi huku majina ya Benki ya Stabink ambao watu walichota pesa kwa maboksi,Sandalusi,magunia ambao wengi wao ni vigogo wakubwa wa ikulu wakiachwa,na ndio maana Ikulu hii inakataza Ripoti ya PCCB iwekwe wazi kwakuwa itaweza kuvuruga nchi kwasababu wahusika waliochota pesa wengi ni watu wa Ikulu”aliongeza Kafulila.
     Kuhusu Jeuri ya Mmiliki wa IPTL Bwana Seith
       Kafulila ambaye  pia ni katibu Mwenezi wa Chama cha NCCR Mageuzi alisema Jeuri aliyekuwa nayo bwana Seith kwa kuzivimbia Mamlaka zote ikiwemo Mamlaka ya ukusanyaji Kodi TRA inatokana na kigogo huyo kufahamu wizi huo ameufanya na vigogo wa kubwa wan chi.
   “Huyu bwana seith anakuwa jeuri sana kwakuwa anauhakika pesa za Escrow amekula na wengi hata akifanya jambo anajua wazi hakuna wakumchukulia hatua kwakuwa wako wengi, na  hii inatokana kutokuwa na serikali makini ndio maana inamuacha huyo taperi kufanya anavyotaka ila serikali ijue huyo mtu avyojisifu hivi atakujakuleta machafuko nchini”alitabainisha Kafulila.
     Katika hatua nyingine Mbunge huyo wa kigoma Kusini alisema kwa sasa chama chake cha NCCR kwa kushikiliana na Umoja wao wa Vyama vya upinzani nchini waanza Rasmi kwenda kwa wananchi kuwaeleza kuhusu suala nzima lilivyo la Escrow na Wamepanga kuanza na Mkoa wa Kigoma.
       “Tuanza tena ziara Mkoani Kigoma kuhamasisha Umma uelewe kuhusu Ufisadi huu,na tunatawajulisha Watanzania kuwa CCM haina uhalali wa kuchaguliwa kwasababu imeshindwa kuisimia serikali yake kwani Makam mwenyekiti Taifa na Katibu wa CCM wamesisitiza kuwa wahusika wawajibike lakini wamegoma”alisema Kafulila 



Posted by Unknown at 04:50
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

About Me

Unknown
View my complete profile

Popular Posts

  • TAZAMA PICHA ZA TUKIO LA UBUNGO
     HUYU NI MMOJAWAPO WA KADA ALIYESHIKA BANGO KATIKA MKUTANO HUO JINA LAKE HALIKUWEZA KUPATIKANA NA DIWAMI WA KATA MAVURUZA BWANA PASCAL ...
  • AJALI YA KUSIKITISHA YATOKEA HUKO BUNJU 'B', DAR ES SALAAM
    Wasamaria wema wakifunuka mwili marehemu baada ya kutoka kwenye jeneza Wasamalia wema wakimmsaidia mume wa marehemu ambaye yupo ta...
  • WAJUMBE WALIORUDI BUNGENI WA UKAWA SIRI ZAO HIZI HAPA
    Na Karoli Vinsent SIRI ya kusalitiwa kwa Wajumbe wanaunda Umoja wa kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA yafichuka mtandao umegundua,Si...
  • MLINZI WA DK SILAA AELEZA UKWELI JUU YA SHTUMA ZAKE
    Mlinzi huyo wakati akizungumza na wanahabari akionyesha majeraha aliyoyapata wakati wa kupokea kipigo hicho Aliyekuwa mlinzi binaf...
  • MWAKYEMBE AFUKUZA 11 UWANJA WA NDEGE LEO
    Waziri wa uchukizi tanzania HARSON MWAKYEMBE akizungumza na wanahabari leo ofisin kwake jijini Dar es salaam              Waziri wa u...
  • RAIS KIKWETE ACHARUKA AWATIMUA KAZI WAKURUGENZI,WAZIRI GHASIA AGOMA KUJIUZULU,ALIVAA GAZETI LA TANZANIA DAIMA SOMA HAPA
    Pichani ni  Waziri  wa Nchi Ofisi ya  Wazir i   Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi)    Hawa Ghasia akizungumza na w...
  • NECTA YATANGAZA MATOKEA,NI IDADI KUBWA YAWANAFUNZI WAFAULU
    Pichani ni Katibu Mkuu wa Baraza la Mitiani nchini NECTA Dkt Charles E Msonde Akizungumza leo na Waandishi wa Habari jijini Dar Es Sa...
  • SOMA HAPA .........................HALI HALISI LA JIMBO LA UBUNGO HII HAPA KWA SIKU YA LEO
    NI WAKATI WA ZIARA YA UKAGUZI WA MAJI NA MIRADI ENDELEVU YA MAJI KATIKA JIMBO LA UBUNGO LIMEZUA HALI YA TAFRANI KWA MBUNGE WA JIMBO HILO MHE...
  • MWIGAMBA;ADUI YANGU SIYO CHADEMA BALI NI CCM
    Na Karoli Vinsent KATIBU mkuu wa chama kipya cha siasa nchini cha   Alliance for Change and Transparence-Tanzania ACT Samsoni Mwigamba ...
  • Unaujua Ugonjwa wa Masundosundo Sehemu za Siri(Genital Warts) soma hapa
      N I vinyama laini vidogo vinavyoota kwenye ngozi au utando laini unaozunguka maeneo ya siri. Vinaweza kutokea kwenye uume, uke, mrija w...

Blog Archive

  • ►  2015 (32)
    • ►  March (9)
    • ►  February (2)
    • ►  January (21)
  • ▼  2014 (145)
    • ▼  December (17)
      • LIGI KUU YA VODACOM YAINGIA RAUNDI YA 9
      • -UKAWA WAMVAA JK,WASEMA MAZITO,DK SLAA AMVAA YEYE ...
      • PUNGUZO KABAMBE ZA TIKETI ZA SAUTI ZA BUSARA KWA W...
      • MATUMIZI YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI
      • SITAJIUZULU MPAKA JK ANIAMBIE;TIBAIJUKA
      • JK AFARIJI FAMILIA YA MWAIBALE,MWILI WASAFIRISHWA ...
      • WEREMA AJIUZULU NAFASI YA MWANASHERIA MKUU WA SERI...
      • RIP AISHA MADINDA
      • Wema Atoa FACT 5 Za Ukweli Kuhusu Zamaradi Mtetema
      • RAIS KIKWETE ACHARUKA AWATIMUA KAZI WAKURUGENZI,WA...
      • Mshindi bora wa ubunifu wa program za simu apatikana
      • 15 KUTOKA NJE WAOMBEWA USAJILI DIRISHA DOGO
      • Na Karoli Vins...
      • MECHI YA NANI MTANI JEMBE KUCHEZWA TAREHE 13 DISEMBA
      • TANZANIA YAUNGANA NA MATAIFA MENGINE KUADHIMISHA M...
      • MAZISHI YA MRAKIBU WA POLISI CAPT.KIDAI SENZALA AL...
      • TAIFA STARS MABORESHO YAINGIA KAMBINI
    • ►  November (36)
    • ►  October (13)
    • ►  September (2)
    • ►  August (20)
    • ►  July (15)
    • ►  June (42)
Simple theme. Theme images by luoman. Powered by Blogger.